Bwana uliyewaita Watakatifu wako, Wawe mitume, wachunga, Walishe kundi lako; wanyonge na wenye hofu Wakawa mashujaa, Na wapole wa kunena Wasiwe kunyamaa. Hata leo wawataka Watakatifu wako, Nawe wauliza tena Ni nani aliyeko Atakaye nimtume Afundishe vijana? 'Ni tayari, Bwana wangu, Nitume mimi Bwana.' Nitume na mimi, Bwana Kama ulivyotumwa, Habari ya msamaha Na dhambi kutubiwa, Niwahubiri wakosa, Na waliopotea, Wokovu u wake Bwana, Aliyewafilia. Astahiliye hapana Kutamka habari, Lakini wewe waweza Kutufanya tayari. Neno lako tulijue, Tupe na roho yako, Hayatakuwa ya bure, Haya maneno yako.عايشين معاك في هنا طفل المغارة Minden örömöm К Тебе я взываю мой Бог Всемогущий Иса Мəсиһ Аллаһын сөзү لا مثل لك - There is none like you Ты для меня свет мира Dalam Roh Yesus Kristus اذا ما غرد العصفور yào zuò xīn zào de rén
Song not available - connect to internet to try again?