Bwana uliyewaita Watakatifu wako, Wawe mitume, wachunga, Walishe kundi lako; wanyonge na wenye hofu Wakawa mashujaa, Na wapole wa kunena Wasiwe kunyamaa. Hata leo wawataka Watakatifu wako, Nawe wauliza tena Ni nani aliyeko Atakaye nimtume Afundishe vijana? 'Ni tayari, Bwana wangu, Nitume mimi Bwana.' Nitume na mimi, Bwana Kama ulivyotumwa, Habari ya msamaha Na dhambi kutubiwa, Niwahubiri wakosa, Na waliopotea, Wokovu u wake Bwana, Aliyewafilia. Astahiliye hapana Kutamka habari, Lakini wewe waweza Kutufanya tayari. Neno lako tulijue, Tupe na roho yako, Hayatakuwa ya bure, Haya maneno yako.Живу Тобой Тәңір Ием арамызда KHRIH NA HLAWT KO RIH عزوا عزوا شعبي Volo per Te mʿ yswʿ T'aimer, ô Sauveur charitable سەن، تەڭىرىم، كۉمۉشتۅن دا اسىل Кутсал Баба Гьоксел Баба Jésus, c'est le plus beau nom
Song not available - connect to internet to try again?