Bwana uliyewaita Watakatifu wako, Wawe mitume, wachunga, Walishe kundi lako; wanyonge na wenye hofu Wakawa mashujaa, Na wapole wa kunena Wasiwe kunyamaa. Hata leo wawataka Watakatifu wako, Nawe wauliza tena Ni nani aliyeko Atakaye nimtume Afundishe vijana? 'Ni tayari, Bwana wangu, Nitume mimi Bwana.' Nitume na mimi, Bwana Kama ulivyotumwa, Habari ya msamaha Na dhambi kutubiwa, Niwahubiri wakosa, Na waliopotea, Wokovu u wake Bwana, Aliyewafilia. Astahiliye hapana Kutamka habari, Lakini wewe waweza Kutufanya tayari. Neno lako tulijue, Tupe na roho yako, Hayatakuwa ya bure, Haya maneno yako.Il me conduit Stal jsi se hříchem Եկել եմ Ներկայությանդ Մեջ قوڭىراۋ ٴان سالادى lḥẓẗ slạm Coronadle Сүйүүң Сенин, Теңир, музду эритет Ty si môj Pastier O, ry mpanota aza manda Куке ти люкаськоды
Song not available - connect to internet to try again?