Bwana wa mabwana, Mwenye nguvu sana Twakusihi: Neno la milele Na liende mbele, Waongoke tele Kwa Mwokozi. Tunaowaona Wanavyopatana, Kulipinga, Hawataliweza Neno, kulitweza: Huwaje! Kucheza: Na upanga? Heri wajitunze Ili wapatane, Na Mwokozi; Watafute sana, Wapate kuona, Yesu kuwa Bwana, Mkombozi. Mungu awaita Wasije kukuta Pigo lake; Hakuona vyema Wakose uzima, Awape rehema, Waokoke. Mwenye utukufu Tunamshukuru Yeye pweke! Nasifiwe sana, Baba, naye Mwana, Na wa tatu tena Roho yake.Кто я для Тебя? nḥn bnw ạlậb ạlrḥym சர்வ சிருஷ்டிக்கும் எஜமானன் நீரே Slnko náš brat O Seigneur, ô Sauveur Венцы Ey Xudo, Mening Yuragim Toc toc chi bussa Жедел хабар Rab, Seninleyim..
Song not available - connect to internet to try again?