Bwana Yesu atakuja, Vumilia! Omba, ukiwa na haja, Vumilia! Mbingunu Mungu aliko, Mwamini Mwokozi wako, Nawe utafika huko, Vumilia! Ikikucheka dunia, Vumilia! Mwovu atakuvizia, Vumilia! Hataweza kukushinda, Bwana Yesu akulinda, Roho yako, akupenda, Vumilia! Na ukiwa hatarini, Vumilia! Dhiki nyingi duniani, Vumilia! Vyatupasa kuyakuta, Majaribu na matata, Na Bwana hakutuficha; Vumilia! Adui wakikutana, Vumilia! Na ndugu wakikukana, Vumilia! Zote, zote zitakwisha, Nguvu zote za kutisha Mungu chini atashusha; Vumilia! Moyoni una majonzi, Vumilia! Ndiyo bonde-ya-machozi, Vumilia! Hima tutaandamana, Kwetu Mbinguni na Bwana Tena hatutaachana; Vumilia!Алыс-шынның Чаяакчызы Бурганымга ạ̉nt tḥbny Исо Масиҳ Подшоҳимиз V zajatí hriechu Bring lof aan die Vader Aujourd'hui tu m'appelles Ишенимдүү Кудайсың Кутсал Танръ Курбанъ Io credo che Аллаһ Оғлуну ҝөндəриб, һалелуја!
Song not available - connect to internet to try again?