Damu imebubujika, Ni ya Imanweli, Wakioga wenye taka, Husafiwa kweli. Ilimpa kushukuru Mwivi mautini; Nami nisiye udhuru, Yanisafi ndani. Kondoo wa kuuawa, Damu ina nguvu, Wako wote kuokoa, Kwa utimilivu. Bwana tangu damu yako Kunisafi kale, Nimeimba sifa zako; Taimba milele. Nikifa tazidi kwimba Sifa za wokovu Ulimi ujaponyamaa Vumbini mwa ufu. Bwana, umenikirimu Nisiyestahili Kwa damu yako, sehemu Ya mali ya kweli. Nikubali kukwimbia, Mbinguni milele, Mungu nitakusifia Jina lako pweke.Salmo 139 Nous entrons dans ta présence الفترة الثالثة 阿爸阿爸我要回家 يا رأسنا الغالي Oram-be mivatravatra arotsahy Tompo o Магтан дуулъя, Израилийн Hai, Puji Namanya Възкръсна силний Спас Pagina bianca
Song not available - connect to internet to try again?