Ni ya Imanweli,
Wakioga wenye taka,
Husafiwa kweli.
Mwivi mautini;
Nami nisiye udhuru,
Yanisafi ndani.
Damu ina nguvu,
Wako wote kuokoa,
Kwa utimilivu.
Kunisafi kale,
Nimeimba sifa zako;
Taimba milele.
Sifa za wokovu
Ulimi ujaponyamaa
Vumbini mwa ufu.
Nisiyestahili
Kwa damu yako, sehemu
Ya mali ya kweli.
Mbinguni milele,
Mungu nitakusifia
Jina lako pweke.