Ewe, Baba wa Mbinguni, Usikie twombalo Hapa chini duniani, Na uwe radhi nalo Ee Mungu, bariki Ndugu hawa wawili! Ee Mungu, bariki Ndugu hawa wawili! Watu hawa mbele zako, Na mbele ya kanisa; Watimize Neno lako Wanakutana sasa. Kama Yesu na Kanisa, Ni mmoja, na hivyo, Watu hawawape sasa Wawe mmoja vivyo Walinde, Bwana, daima, Wabariki nyumbani Uwape nyingi salama Humu ulimwenguni. Wabariki, ewe Bwana, Watu hawa wawili, Wape upaji wa wana, Wafurahishwe kweli. Siku za duniani Zitakapopungua, Wape kurithi Mbinguni Mema ya kwendelea.ạllh ṭryqh kạml bḥb ạlrb Доноликнинг Баракаси Однажды средь ночи учитель в тиши Loué soit Dieu, le Seigneur Halliluyya! СЪРЦЕ ЧИСТО СЪТВОРИ В МЕН В тени крыл Его святых For all the saints/ Sine Nomine On My Side
Song not available - connect to internet to try again?