Kazi yangu ikiisha, nami nikiokoka; Na kuvaa kutokuharibika, Nitamjua Mwokozi nifikapo ng'amboni; Atakuwa wa kwanza kunilaki. Nitamjua, nitamjua, nikimwona uso kwa uso; Nitamjua, nitamjua, kwa alama za misumari. Furaha nitapata nikiona makao Bwana aliyotuandalia; Nitamsifu mwokozi kwa rehema na pendo Vilivyonipa pahali Mbinguni. Nao waliokufa katika Bwana Yesu, Nitawaona tena huko juu; Lakini nifikapo kwake huko Mbinguni, Nataka kumwona Mwokozi kwanza. Milangoni mwa mji Bwana atanipitisha, Pasipo machozi wala huzuni. Nitauimba wimbo wa milele; lakini Nataka kumwona Mwokozi kwanza.قد علمت Choinek blask Сабахлайън калктън мъ Smieť žiť pre Krista Сохрани страну мою سِنگ اُنگونگده باش اِگیَن Davanti al trono Kríž je znakom spásy الىسقى بەيت۔لەحەمدە، حان سارايدا ەمەس Praise The Lord, O My Soul - 我的心,你要稱頌耶和華
Song not available - connect to internet to try again?