Kazi yangu ikiisha, nami nikiokoka; Na kuvaa kutokuharibika, Nitamjua Mwokozi nifikapo ng'amboni; Atakuwa wa kwanza kunilaki. Nitamjua, nitamjua, nikimwona uso kwa uso; Nitamjua, nitamjua, kwa alama za misumari. Furaha nitapata nikiona makao Bwana aliyotuandalia; Nitamsifu mwokozi kwa rehema na pendo Vilivyonipa pahali Mbinguni. Nao waliokufa katika Bwana Yesu, Nitawaona tena huko juu; Lakini nifikapo kwake huko Mbinguni, Nataka kumwona Mwokozi kwanza. Milangoni mwa mji Bwana atanipitisha, Pasipo machozi wala huzuni. Nitauimba wimbo wa milele; lakini Nataka kumwona Mwokozi kwanza.О, прыгажэйшы з сыноў чалавечых Svou sílu dej nám ПРИБЕЖИЩЕ СИ Карнайлар садоси билан Раб'де Хузур Бул Chwalmy Pana wszyscy Gloria al Padre y al Hijo Ich brauch dich allezeit Chihowa yʋt binili ka Лишь любовь Твоя
Song not available - connect to internet to try again?