Kazi yangu ikiisha, nami nikiokoka; Na kuvaa kutokuharibika, Nitamjua Mwokozi nifikapo ng'amboni; Atakuwa wa kwanza kunilaki. Nitamjua, nitamjua, nikimwona uso kwa uso; Nitamjua, nitamjua, kwa alama za misumari. Furaha nitapata nikiona makao Bwana aliyotuandalia; Nitamsifu mwokozi kwa rehema na pendo Vilivyonipa pahali Mbinguni. Nao waliokufa katika Bwana Yesu, Nitawaona tena huko juu; Lakini nifikapo kwake huko Mbinguni, Nataka kumwona Mwokozi kwanza. Milangoni mwa mji Bwana atanipitisha, Pasipo machozi wala huzuni. Nitauimba wimbo wa milele; lakini Nataka kumwona Mwokozi kwanza.جانارىما انىقتاپ زەر سال اسپان كوزىمەن Ханлтан өргҗәнәв Con te Кутсал, Кутсал, Кутсал, Раб Аллах Хейбетли! Vydaj sa úprimne Pánovi! Чем могу воздать ياللى بديت الرحلة معايا Salvación para el perdido Дыханье ветра на губах ربي بحبك من كل قلبي
Song not available - connect to internet to try again?