Kazi yangu ikiisha, nami nikiokoka; Na kuvaa kutokuharibika, Nitamjua Mwokozi nifikapo ng'amboni; Atakuwa wa kwanza kunilaki. Nitamjua, nitamjua, nikimwona uso kwa uso; Nitamjua, nitamjua, kwa alama za misumari. Furaha nitapata nikiona makao Bwana aliyotuandalia; Nitamsifu mwokozi kwa rehema na pendo Vilivyonipa pahali Mbinguni. Nao waliokufa katika Bwana Yesu, Nitawaona tena huko juu; Lakini nifikapo kwake huko Mbinguni, Nataka kumwona Mwokozi kwanza. Milangoni mwa mji Bwana atanipitisha, Pasipo machozi wala huzuni. Nitauimba wimbo wa milele; lakini Nataka kumwona Mwokozi kwanza.Il senso della vita Суруди Ҳанно Jezus, Jezus تولتۇرغىن موشۇ جاينى كللت السنة بجودك hạṣdq ạ̹nk ḥy Chváľ Pána, duša moja, haleluja! యేసుతో ఠీవిగాను పోదమా Әсләйли Рәбни Ku komu pôjdem
Song not available - connect to internet to try again?