Kazi yangu ikiisha, nami nikiokoka; Na kuvaa kutokuharibika, Nitamjua Mwokozi nifikapo ng'amboni; Atakuwa wa kwanza kunilaki. Nitamjua, nitamjua, nikimwona uso kwa uso; Nitamjua, nitamjua, kwa alama za misumari. Furaha nitapata nikiona makao Bwana aliyotuandalia; Nitamsifu mwokozi kwa rehema na pendo Vilivyonipa pahali Mbinguni. Nao waliokufa katika Bwana Yesu, Nitawaona tena huko juu; Lakini nifikapo kwake huko Mbinguni, Nataka kumwona Mwokozi kwanza. Milangoni mwa mji Bwana atanipitisha, Pasipo machozi wala huzuni. Nitauimba wimbo wa milele; lakini Nataka kumwona Mwokozi kwanza.ạnhḍ Wiem nie zawiedzie mnie Pan sòng gěi qí dǎo de mǔ qīn Тюм ЬОвгю Beytlehem Kom til din frelser ПОМНИ ЧЕ ТИ في الخوف إنت سلامي من حبك للعالم 主这是你的身体
Song not available - connect to internet to try again?