Kazi yangu ikiisha, nami nikiokoka; Na kuvaa kutokuharibika, Nitamjua Mwokozi nifikapo ng'amboni; Atakuwa wa kwanza kunilaki. Nitamjua, nitamjua, nikimwona uso kwa uso; Nitamjua, nitamjua, kwa alama za misumari. Furaha nitapata nikiona makao Bwana aliyotuandalia; Nitamsifu mwokozi kwa rehema na pendo Vilivyonipa pahali Mbinguni. Nao waliokufa katika Bwana Yesu, Nitawaona tena huko juu; Lakini nifikapo kwake huko Mbinguni, Nataka kumwona Mwokozi kwanza. Milangoni mwa mji Bwana atanipitisha, Pasipo machozi wala huzuni. Nitauimba wimbo wa milele; lakini Nataka kumwona Mwokozi kwanza.Ascolta ogni battito رفعت عيني tʿlyq 4 - ạ̹sẖfyny Алғыс Саған - Тәңир! mḥbẗ ạlmsyḥ Биз тетик борамиз Oh santísimo, felicísimo We Cry Out Dejad a los niños, niños Ходить в собрание - не значит Бога знать
Song not available - connect to internet to try again?