Kazi yangu ikiisha, nami nikiokoka; Na kuvaa kutokuharibika, Nitamjua Mwokozi nifikapo ng'amboni; Atakuwa wa kwanza kunilaki. Nitamjua, nitamjua, nikimwona uso kwa uso; Nitamjua, nitamjua, kwa alama za misumari. Furaha nitapata nikiona makao Bwana aliyotuandalia; Nitamsifu mwokozi kwa rehema na pendo Vilivyonipa pahali Mbinguni. Nao waliokufa katika Bwana Yesu, Nitawaona tena huko juu; Lakini nifikapo kwake huko Mbinguni, Nataka kumwona Mwokozi kwanza. Milangoni mwa mji Bwana atanipitisha, Pasipo machozi wala huzuni. Nitauimba wimbo wa milele; lakini Nataka kumwona Mwokozi kwanza.Ben Severim Rabbimi ạ̉nạ bdy ạ̉qḍy ạ̉wqạty تەڭىر ىيسا قادالدى ايقاش جىعاچقا Nazioni per Cristo 别怕路艰难 THE SOLID ROCK لهيب حبك يسعدني Сəнə, Хиласкарым, мөһтаҹам Тюм варлъъмъ даатсам Мерхаметли Бир Танръ
Song not available - connect to internet to try again?