Msingi imara, enyi wa kweli, Umekwisha pigwa kwa neno hili; Aongeze lipi? Mnayo pia Kwa Yesu mliomkimbilia. Wambiwapo vuka maji ya giza, Mito ya mashaka taipunguza; Takupa nawe, nikuwezeshe, Ipata kufaa, isikutishe! Utakapopishwa ndani ya moto Nnguvu nitakupa, upate pato; Huteketezwi, ila taka zako, Na zitasalia dhahabu zako. Hata zije mvi, walio wangu Hawaoni kwisha mapenzi yangu; Nazo zitakapowenea, ndipo Mabegani mwangu niwatwekapo. Na mtu aliyenitegemea Kamwe kwa adui sitamtia; Nguvu za jehanam zijapotisha, Mtu wangu kamwe sitamuacha.Alors je verrai face à face مادمت ربي في الطريق wǒ de zhǔ wǒ xīn ài nǐ పరలోకము నా దేశము Un enfant si petit Раб'де Даима Севинин Kasih Tuhanku Veľkú milosť udeľuješ Özlemim Tek Sana Ait ạʿln ạ̹njyl ạlḥb
Song not available - connect to internet to try again?