Tangu siku hiyo aliponijia, Akae moyoni mwangu, Sina giza tena, ila mwanga pia Kwa Yesu mwokozi wangu. Amani moyoni mwangu, kwa Yesu, Mwokozi wangu; Sina shaka kamwe, Kwa sababu yeye, Yu nami moyoni mwangu. Sina haja tena, ya kutanga-tanga, Ndiye kiongozi wangu. Dhambi zangu zote zimeondolewa, Na Yesu, Mwanawe Mungu. Matumaini yangu ni ya hakika, Katika Mwokozi wangu. Hofu zangu na hamu zimeondoka, kwa kuwa ninaye Yesu. Siogopi tena, nikiitwa kufa, Yu nami daima, Yesu. Mlango wa Mbinguni ni yeye pia, 'Tapita humo kwa damu.' Nitaketi na yeye huko milele, Nisifu Mwokozi wangu. Nina raha moyoni majira yote, Kwa Yesu, Mwanawe Mungu.Ха Халелуя Któż jest tak święty Сенин Севгин бюйюктюр K večeru sa deň nachýlil مسيحي للأرض جيت Sevgi Kaynağı Ti do la gloria jạnạ m ạlsmạ jạnạ Už skvie sa ráno vzkriesenia - Haleluja Раб Чобанъмдър, Ексиим Олмаз
Song not available - connect to internet to try again?