Tangu siku hiyo aliponijia, Akae moyoni mwangu, Sina giza tena, ila mwanga pia Kwa Yesu mwokozi wangu. Amani moyoni mwangu, kwa Yesu, Mwokozi wangu; Sina shaka kamwe, Kwa sababu yeye, Yu nami moyoni mwangu. Sina haja tena, ya kutanga-tanga, Ndiye kiongozi wangu. Dhambi zangu zote zimeondolewa, Na Yesu, Mwanawe Mungu. Matumaini yangu ni ya hakika, Katika Mwokozi wangu. Hofu zangu na hamu zimeondoka, kwa kuwa ninaye Yesu. Siogopi tena, nikiitwa kufa, Yu nami daima, Yesu. Mlango wa Mbinguni ni yeye pia, 'Tapita humo kwa damu.' Nitaketi na yeye huko milele, Nisifu Mwokozi wangu. Nina raha moyoni majira yote, Kwa Yesu, Mwanawe Mungu.يا كل ملوك الأرض W trzecim rozdziale napisał nam Jan Senga berildi imkon Ó, nebo už v srdci mám يسوع ربي Reign in Us 일어나라 주의 백성 Môj Boh, vďaka Tebe dýcham Kim inanırsa İsa Mesih'e Čo chce môj Boh
Song not available - connect to internet to try again?