Namwndama Bwana kwa alilonena Njia yangu huning'azia; Nikimridhisha atanidumisha Taamini nitii pia. Amini utii, njia pweke ni hii Ya furaha kwa Yesu: amini ukatii. Giza sina kwangu wala hata wingu Yeye mara huviondoa Woga, wasiwasi, sononeko, basi; Huamini nitii pia. Masumbuko yote, sikitiko lote; Kwa mapenzi hunilipia; Baa, dhara, dhiki, vivyo hubariki Taamini nitii pia. Mimi sitajua raha sawasawa Ila yote Yesu kumpa; Napata fadhili na radhi kamili, Taamini nitii pia. Nitamfurahia na kumtumaini, Majumbani na njia-njia; Agizo natenda, nikitumwa hwenda, Huamini nitii pia.Sin Deus nada somos Nem vagyok rá méltó A ti mi voz elevo Jeg er lykkelig. حزن وشدة وضيق Nu ne lasa sa ne-ndoim Hosanna Libero Głos Jezusa słychać Сердце чистое не плачет
Song not available - connect to internet to try again?