Naweka dhambi zangu Juu yake Bwana Kuziondoa, kwangu Hulemea sana; Na uaili wangu Ameuondoa; Dawa yangu ni damu, Kwa hiyo napoa. Na uhitaji wangu Nitamjuvisha Kwa upungufu wangu Yeye anatosha; Majonzi yangu yote Na mizigo yangu, Atachukua vyote Yesu Bwana wangu. Na roho yangu nayo, Imechoka sana; Namletea hiyo Ilindwe na Bwana; Ni jema jina lake, Nalo lapendeza, Imanweli na kwake tutalitukuza. Natamani daima Niwe kama Bwana, Mpole, tena mwema, Wa mapenzi sana; Zaidi natamani Kwenda kwake juu, Nikaone mbinguni Enzi yake kuu.nạẓrạaⁿ ạ̹lyk أما أنا فبكثرة رحمتك yạ mn tkẖyr Изливай hwdẖạ qd ṣạr lyl mẓlm Du får koma til Jesus Salut, blanche étoile По-близо Svätý, svätý, svätý je náš Boh všemohúci Ыйса, ачтың чындыкты Сен
Song not available - connect to internet to try again?