Naweka dhambi zangu Juu yake Bwana Kuziondoa, kwangu Hulemea sana; Na uaili wangu Ameuondoa; Dawa yangu ni damu, Kwa hiyo napoa. Na uhitaji wangu Nitamjuvisha Kwa upungufu wangu Yeye anatosha; Majonzi yangu yote Na mizigo yangu, Atachukua vyote Yesu Bwana wangu. Na roho yangu nayo, Imechoka sana; Namletea hiyo Ilindwe na Bwana; Ni jema jina lake, Nalo lapendeza, Imanweli na kwake tutalitukuza. Natamani daima Niwe kama Bwana, Mpole, tena mwema, Wa mapenzi sana; Zaidi natamani Kwenda kwake juu, Nikaone mbinguni Enzi yake kuu.Veloma no apetrako Kdybych já byl motýlkem rbnạ .. rbnạ zy mạ ʿyn ạlbyby Manenoa, ry farara Яшна wǒ yào zhàn zài shén de huà yǔ shàng Tak veľa dôvodov mám wǒ yǒu yī wèi shén Аз пея с радост за Голгота
Song not available - connect to internet to try again?