Naweka dhambi zangu Juu yake Bwana Kuziondoa, kwangu Hulemea sana; Na uaili wangu Ameuondoa; Dawa yangu ni damu, Kwa hiyo napoa. Na uhitaji wangu Nitamjuvisha Kwa upungufu wangu Yeye anatosha; Majonzi yangu yote Na mizigo yangu, Atachukua vyote Yesu Bwana wangu. Na roho yangu nayo, Imechoka sana; Namletea hiyo Ilindwe na Bwana; Ni jema jina lake, Nalo lapendeza, Imanweli na kwake tutalitukuza. Natamani daima Niwe kama Bwana, Mpole, tena mwema, Wa mapenzi sana; Zaidi natamani Kwenda kwake juu, Nikaone mbinguni Enzi yake kuu.İster Misin Günahtan Arınmak? Օրհնություն Քեզ Умудум О'ндадър Безграничный Бог Я Тобою живу ما أحلى الإخوة yạạ̹lhy̱ lạ tnsạny Tezde yavrum benim yạlly mʿạk ạlrḥlẗ Čím väčší kríž, tým bližšie nebo
Song not available - connect to internet to try again?