Naweka dhambi zangu Juu yake Bwana Kuziondoa, kwangu Hulemea sana; Na uaili wangu Ameuondoa; Dawa yangu ni damu, Kwa hiyo napoa. Na uhitaji wangu Nitamjuvisha Kwa upungufu wangu Yeye anatosha; Majonzi yangu yote Na mizigo yangu, Atachukua vyote Yesu Bwana wangu. Na roho yangu nayo, Imechoka sana; Namletea hiyo Ilindwe na Bwana; Ni jema jina lake, Nalo lapendeza, Imanweli na kwake tutalitukuza. Natamani daima Niwe kama Bwana, Mpole, tena mwema, Wa mapenzi sana; Zaidi natamani Kwenda kwake juu, Nikaone mbinguni Enzi yake kuu.Знаешь ли ручей زمن التعويضات O, szczęśliwa noc Figli nel sole ТЕБ МОЛИМ ОТЧЕ НАШ Збережу Perché è degno เชื่อฤทธิ์พระโลหิต If that isn't love When I bow
Song not available - connect to internet to try again?