Nilikuwa kondoo aliyepotea, Sikupenda zizi kamwe, ila kutembea Nilikuwa mwana asiyesikia, Sikupenda baba yangu wala kutulia. Na mchunga mwema alinitafuta, Baba kwa mapenzi ndiye aliyenivuta; Karibu ya kufa, kwa kiu na kwa njaa, Waliniona mnyonge, waliniokoa. Yesu ni mchunga, mwenziwe hapana, Aliosha taka zangu, dhambi nyingi sana; Kwa vidonda vyangu alitia dawa. Ndiye aliyenipata, na kwake nalindwa. Nilikuwa kondoo aliyepotea Sasa nampenda Baba, na mchunga pia; Kwanza nilitanga na kukosa sana, Hivi nyumbani mwa Baba sipotei tena.Страха не хочу иметь Ježiš, najkrajšie meno L'Eternel est mon Berger The head that once was crowned/ St. Magnus/ St. Fulbert На самотi чекаю я на Тебе ạ̉nạ mḥbwb jdaⁿạ jdaⁿạ ʿmr ạltlmydẖ sydy hạ ạ̉nạ Vím, že Ježíš miluje mne Я хочу быть Твоим мой Господь дорогой
Song not available - connect to internet to try again?