Nilikuwa kondoo aliyepotea, Sikupenda zizi kamwe, ila kutembea Nilikuwa mwana asiyesikia, Sikupenda baba yangu wala kutulia. Na mchunga mwema alinitafuta, Baba kwa mapenzi ndiye aliyenivuta; Karibu ya kufa, kwa kiu na kwa njaa, Waliniona mnyonge, waliniokoa. Yesu ni mchunga, mwenziwe hapana, Aliosha taka zangu, dhambi nyingi sana; Kwa vidonda vyangu alitia dawa. Ndiye aliyenipata, na kwake nalindwa. Nilikuwa kondoo aliyepotea Sasa nampenda Baba, na mchunga pia; Kwanza nilitanga na kukosa sana, Hivi nyumbani mwa Baba sipotei tena.Beni Sevdiğin Gibi JESUH NIH A KAN CEUTER Blessing, Honor, Glory اللي اتولدوا هو ملك الملوك في منزل وسط الجليل Господь - твой Бог среди тебя Men baxtliman yakshanbada Indreapta-mi spre Tine inima 何等荣耀
Song not available - connect to internet to try again?