Nilikuwa kondoo aliyepotea, Sikupenda zizi kamwe, ila kutembea Nilikuwa mwana asiyesikia, Sikupenda baba yangu wala kutulia. Na mchunga mwema alinitafuta, Baba kwa mapenzi ndiye aliyenivuta; Karibu ya kufa, kwa kiu na kwa njaa, Waliniona mnyonge, waliniokoa. Yesu ni mchunga, mwenziwe hapana, Aliosha taka zangu, dhambi nyingi sana; Kwa vidonda vyangu alitia dawa. Ndiye aliyenipata, na kwake nalindwa. Nilikuwa kondoo aliyepotea Sasa nampenda Baba, na mchunga pia; Kwanza nilitanga na kukosa sana, Hivi nyumbani mwa Baba sipotei tena.Раббим Сени олқишлашни истайман В духе взгляни на вершину Голгофы Agneau de Dieu, messager de la grâce المسيح اليوم قام yswʿnạ ạtwld و، قۇداي، سەنى ويلايمىن في قلبي شكر وتسبيح Iso shuhrat Podshohi Jeg elsker Jesus lyk fy̱ qlby
Song not available - connect to internet to try again?