Nipe moyo wenye sifa Sio wa utumwa; Moyo ulionyunyizwa Damu ya thamani. Moyo msikizi, moyo Wa kunyenyekea, Moyo utawaliwao Na Mwokozi pia. Mwenye kutubu, mnyonge, Sadiki, amini; Kamwe, kamwe asitengwe Akaaye ndani. Mpya, mwema na mawazo Mwingi wa mapenzi Nawe uwe kielelezo Moyo wa Mwokozi. Ni uule moyo wako; Moyo wa huruma Yesu, natamani kwako Kukujua vyema. Na ya midomo matunda Yako, nipe nami; Amani isiyokoma Iwe yangu mimi. Nitie yako tabia, Inishukie juu; Jina lako nipe pia, Ndilo la upendo. Ni wa baba utukufu; Mwana atukuke; Na roho Mtakatifu U utatu pweke.Na rukách ťa prenesiem ربنا يسوع آتي Oxuyacam bütün ömrüm boyu Время уходит столетья уносит Don't you want to go to Heaven Ostanem stáť, pevne stáť Our Father Isoyim Najotkorim Вера моя Hospodine, přišli sme Tě chválit
Song not available - connect to internet to try again?