Njoni!Njoni!Wenye dhambi, Njoni, msikawie; Yesu anawangojea ndiye awapendaye; Ajuaye awezaye kuwaponya ni Yeye. Ajuaye awezaye kuwaponya ni Yeye. Ewe muhitaji uje; Anakukaribisha, Imani, kweli, na toba, Neema ya kutosha, Jua sana, kwake Bwana Bure utapata. Njoni, mliolemewa Na dhambi ya Adamu; Mkingoja kujiponya Mtapotea mumu; Si wa haki, ni wakosa Waoshwao kwa damu. Ikamtokea dhiki, Mle Gethisemani; Kisha alipoangikwa Akalia mtini; ' Imekwisha', alitosha Dhabihu ya thamani. Kristo aliye Mbinguni Hutuombea huko; Basi mtumai yeye; Kamwe mwingine hako Yesu pweke, Yesu pweke, Ndiye Mwokozi wako. Wamsifu-sifu sana Mbinguni malaika; Wachanganya nyimbo zao Na waliookoka: Aleluya wataimba Waliooshwa taka.Tu sei santo Voi tutti che siete assetati في ابنه Imoningdan qaytmagin yạ sydy lmạ ạ̉ry̱ njwmk حبيبي يا يسوع Dari IV Track 06 Сакън Умудун Кайбетме غابت الشمس Иса бизе кувветлидир
Song not available - connect to internet to try again?