Njoni!Njoni!Wenye dhambi, Njoni, msikawie; Yesu anawangojea ndiye awapendaye; Ajuaye awezaye kuwaponya ni Yeye. Ajuaye awezaye kuwaponya ni Yeye. Ewe muhitaji uje; Anakukaribisha, Imani, kweli, na toba, Neema ya kutosha, Jua sana, kwake Bwana Bure utapata. Njoni, mliolemewa Na dhambi ya Adamu; Mkingoja kujiponya Mtapotea mumu; Si wa haki, ni wakosa Waoshwao kwa damu. Ikamtokea dhiki, Mle Gethisemani; Kisha alipoangikwa Akalia mtini; ' Imekwisha', alitosha Dhabihu ya thamani. Kristo aliye Mbinguni Hutuombea huko; Basi mtumai yeye; Kamwe mwingine hako Yesu pweke, Yesu pweke, Ndiye Mwokozi wako. Wamsifu-sifu sana Mbinguni malaika; Wachanganya nyimbo zao Na waliookoka: Aleluya wataimba Waliooshwa taka.Unknown На небесната проверка kẖlny qrb ạlṣlyb ИСУС - НАЙ-ДИВНО ИМЕ Teńdesi joq Uly Qudaı Fraţi surori cântaţi Я иду к отчизне к той стране ḍllt ạlṭryq wǒ yǐ jīng dǒng dé zěn yàng qù xuǎn zé Nel suo amore
Song not available - connect to internet to try again?