Njoni!Njoni!Wenye dhambi, Njoni, msikawie; Yesu anawangojea ndiye awapendaye; Ajuaye awezaye kuwaponya ni Yeye. Ajuaye awezaye kuwaponya ni Yeye. Ewe muhitaji uje; Anakukaribisha, Imani, kweli, na toba, Neema ya kutosha, Jua sana, kwake Bwana Bure utapata. Njoni, mliolemewa Na dhambi ya Adamu; Mkingoja kujiponya Mtapotea mumu; Si wa haki, ni wakosa Waoshwao kwa damu. Ikamtokea dhiki, Mle Gethisemani; Kisha alipoangikwa Akalia mtini; ' Imekwisha', alitosha Dhabihu ya thamani. Kristo aliye Mbinguni Hutuombea huko; Basi mtumai yeye; Kamwe mwingine hako Yesu pweke, Yesu pweke, Ndiye Mwokozi wako. Wamsifu-sifu sana Mbinguni malaika; Wachanganya nyimbo zao Na waliookoka: Aleluya wataimba Waliooshwa taka.تعليق 11 - مين الكسبان ؟ Te-am inteles dar nu deajuns Иисус - Царь благодати Притчи కనుచూపుమేరలోన ఏ ఆశలేని వేళ Aandgesang Dios eterno en tu presencia ạ̹lqạʾ 7 Najlepszy z wszystkich przyjaciel Грозные тучи нависли над нами
Song not available - connect to internet to try again?