Siku ya Mbinguni kujawa na sifa, Dhambi zilizidi duniani; Yesu akaja azaliwe mtu, Awe na watu ulimwenguni. Alinipenda, alinifia, Ameondoa na dhambi zangu; Alifufuka nipewe haki, Yuaja tena Mwokozi wangu. Na siku moja walikwenda naye, Wakamkaza msalabani; Aliumia, aliaibishwa, Ili atuokoe dhambini. Siku hiyo wakamlaza chini Kaburini alipumzika; Matumaini yetu wenye dhambi, Ni mwokozi, kwake twaokoka. Kaburi likashindwa kumshika; Jiwe likatoka mlangoni, Alifufuka kwa kushinda kwake, Naye yuko milele Mbinguni. Siku moja atatujia tena; Utukufu wake tutaona; Atawaleta na wapenzi wetu; Mwokozi: wangu, tutaonana.Ráč naše deti sám Buď slaven, lásky zdroji Bizi Seviyorsun Ya Rab يا كاشف 以色列啊你要听着 Спасен Degno in Te యుద్ధము యెహోవాదే Přijmi, Pane, život můj Cantiamo con gioia
Song not available - connect to internet to try again?