Siku ya Mbinguni kujawa na sifa, Dhambi zilizidi duniani; Yesu akaja azaliwe mtu, Awe na watu ulimwenguni. Alinipenda, alinifia, Ameondoa na dhambi zangu; Alifufuka nipewe haki, Yuaja tena Mwokozi wangu. Na siku moja walikwenda naye, Wakamkaza msalabani; Aliumia, aliaibishwa, Ili atuokoe dhambini. Siku hiyo wakamlaza chini Kaburini alipumzika; Matumaini yetu wenye dhambi, Ni mwokozi, kwake twaokoka. Kaburi likashindwa kumshika; Jiwe likatoka mlangoni, Alifufuka kwa kushinda kwake, Naye yuko milele Mbinguni. Siku moja atatujia tena; Utukufu wake tutaona; Atawaleta na wapenzi wetu; Mwokozi: wangu, tutaonana.Jeruzalemie, grodzie mój Нууцлагхан чимээгүй газар mwsyqy ạlmqdmẗ - tẖmr sẖfạh 1 ạ̹nt ạllḥn ạlly bạgẖnyh Ումն է Մեծ Փառքը كيەلى رۋح إنت فين Noche de paz Hiçbir Şeyde Kaygı Çekmeyin Мəн Сəни севирəм
Song not available - connect to internet to try again?