Siku ya Mbinguni kujawa na sifa, Dhambi zilizidi duniani; Yesu akaja azaliwe mtu, Awe na watu ulimwenguni. Alinipenda, alinifia, Ameondoa na dhambi zangu; Alifufuka nipewe haki, Yuaja tena Mwokozi wangu. Na siku moja walikwenda naye, Wakamkaza msalabani; Aliumia, aliaibishwa, Ili atuokoe dhambini. Siku hiyo wakamlaza chini Kaburini alipumzika; Matumaini yetu wenye dhambi, Ni mwokozi, kwake twaokoka. Kaburi likashindwa kumshika; Jiwe likatoka mlangoni, Alifufuka kwa kushinda kwake, Naye yuko milele Mbinguni. Siku moja atatujia tena; Utukufu wake tutaona; Atawaleta na wapenzi wetu; Mwokozi: wangu, tutaonana.عرس الحمل Братья сестры дружно смело Anche se ci son le nuvole mwsyqy̱ Dico sì sbḥwạ ạllh bqdsh I REMEMBER EDEN Сээӊ ынакшылыӊ кызыгаары чок Верен Бог имам аз Теплий дощ
Song not available - connect to internet to try again?