Siku ya Mbinguni kujawa na sifa, Dhambi zilizidi duniani; Yesu akaja azaliwe mtu, Awe na watu ulimwenguni. Alinipenda, alinifia, Ameondoa na dhambi zangu; Alifufuka nipewe haki, Yuaja tena Mwokozi wangu. Na siku moja walikwenda naye, Wakamkaza msalabani; Aliumia, aliaibishwa, Ili atuokoe dhambini. Siku hiyo wakamlaza chini Kaburini alipumzika; Matumaini yetu wenye dhambi, Ni mwokozi, kwake twaokoka. Kaburi likashindwa kumshika; Jiwe likatoka mlangoni, Alifufuka kwa kushinda kwake, Naye yuko milele Mbinguni. Siku moja atatujia tena; Utukufu wake tutaona; Atawaleta na wapenzi wetu; Mwokozi: wangu, tutaonana.Senin Gibi /11 Nech pokoj Boží Jesus on the inside سېنىڭ نامىڭ قۇدرەتلىك Cristo RE-P Не Мюкеммел Адъндър Utíšme plač v smutnej chvíli Ora confido in te (Salmo 13) Nu te-ndoi ci crede Do mesta Betlema pospiechajme
Song not available - connect to internet to try again?