Waimba, sikizeni, Malaika Mbinguni; Wimbo wa tamu sana Wa pendo zake Bwana, 'Duniani salama, Kwa wakosa rehema.' Sisi sote na twimbe Nao wale wajumbe; Waimba, sikizeni, Malaika mbinguni. Ndiye Bwana wa Mbingu, Tangu milele Mungu, Amezaliwa mwili, Mwana wa mwanamwali; Ametoka enzini Kuja ulimwenguni Mwokozi atufie, Ili tusipotee. Waimba, sikizeni, Malaika Mbinguni. Mtukufu wa amani Ametoka Mbinguni, Jua la haki, ndiye Atumulikiaye; Amejivua enzi, Alivyo na mapenzi, Ataka kutuponya, Kutuzalisha upya, Waimba sikizeni, Malaika Mbinguni. Njoo upesi, Bwana, Twakutamani sana; Kaa nasi, mwokozi Vita hatuviwezi; Vunja kichwa cha nyoka, Sura zako andika, Tufanane na wewe, Kwetu sifa upewe, Waimba, sikizeni, Malaika Mbinguni.پەندە ەمەس قوي جاراتۋشى ربي نور بنورك فيَّ أتي إليك حبيبي О, Енэжвывса миян Бать O Dieu! ta loi est sainte ạ̹nt ạlsẖạfy lmntẓrynk Am auzit că ai murit pe-o cruce Jeg løfter mine øyne Не вставайте так быстро с молитвы Наполняй Дух Святой
Song not available - connect to internet to try again?