Waimba, sikizeni, Malaika Mbinguni; Wimbo wa tamu sana Wa pendo zake Bwana, 'Duniani salama, Kwa wakosa rehema.' Sisi sote na twimbe Nao wale wajumbe; Waimba, sikizeni, Malaika mbinguni. Ndiye Bwana wa Mbingu, Tangu milele Mungu, Amezaliwa mwili, Mwana wa mwanamwali; Ametoka enzini Kuja ulimwenguni Mwokozi atufie, Ili tusipotee. Waimba, sikizeni, Malaika Mbinguni. Mtukufu wa amani Ametoka Mbinguni, Jua la haki, ndiye Atumulikiaye; Amejivua enzi, Alivyo na mapenzi, Ataka kutuponya, Kutuzalisha upya, Waimba sikizeni, Malaika Mbinguni. Njoo upesi, Bwana, Twakutamani sana; Kaa nasi, mwokozi Vita hatuviwezi; Vunja kichwa cha nyoka, Sura zako andika, Tufanane na wewe, Kwetu sifa upewe, Waimba, sikizeni, Malaika Mbinguni.NA NGAIHCHIATNAK HLAW TUAH Яви нам милость Chvíle najvzácnejšie prežívam Исо بئر تۇۇعاندار، تەڭىر بئزدى Кәлдим бүгүн Bože si povedal هللي نفسي وغني Let Your Kingdom Come Highest
Song not available - connect to internet to try again?