Waimba, sikizeni, Malaika Mbinguni; Wimbo wa tamu sana Wa pendo zake Bwana, 'Duniani salama, Kwa wakosa rehema.' Sisi sote na twimbe Nao wale wajumbe; Waimba, sikizeni, Malaika mbinguni. Ndiye Bwana wa Mbingu, Tangu milele Mungu, Amezaliwa mwili, Mwana wa mwanamwali; Ametoka enzini Kuja ulimwenguni Mwokozi atufie, Ili tusipotee. Waimba, sikizeni, Malaika Mbinguni. Mtukufu wa amani Ametoka Mbinguni, Jua la haki, ndiye Atumulikiaye; Amejivua enzi, Alivyo na mapenzi, Ataka kutuponya, Kutuzalisha upya, Waimba sikizeni, Malaika Mbinguni. Njoo upesi, Bwana, Twakutamani sana; Kaa nasi, mwokozi Vita hatuviwezi; Vunja kichwa cha nyoka, Sura zako andika, Tufanane na wewe, Kwetu sifa upewe, Waimba, sikizeni, Malaika Mbinguni.Ry Jesosy Tomponay Для Бога жить святое приглашенье Наш Отец - Бог Иса Яшъйор НЕЖНО МОЕТО СЪРЦЕ Весна вновь наш край посетила Navnet Jesus blekner aldri Gałązka drobna, wątła z Jessego trysła pnia Hayot Kitobi Севгин Ен Йюксек Дадан Даха Йюджедир
Song not available - connect to internet to try again?