Waponyeni watu wamo kifoni, Watoeni walio shimoni; Na aangukaye mumzuie; Ya Bwana Yesu wahubirini. Walio kifoni waokoeni, Mwokozi yuko, wahubirini. Wajapokawia anangojea, Awasubiri waje tobani; Msiwadharau, muwaonyeni; Huwasamehe; wakiamini. Myoyoni mwa ndani, yule shetani Ameyaseta mawazo yao; Lakini kwa Bwana huwa mazima, Tukiwavuta kwa pole hao. Kawaokoeni, wale njiani, Mutimize mapenzi ya Bwana; Na kwa nguvu zake warudi kwake, Kwa subira waonyeni sana.İsa, İsa Yücesin ạllh byḥbny lạ tkẖạf Rey de reyes, Señor de señores kl ḥmdy Ry Jesosy, Izay Mpiahy Пусть никто о Боге нам не скажет À jamais سەندەن مەنى اجىراتپاسىن శృతిచేసి నే పాడనా స్తోత్ర గీతం
Song not available - connect to internet to try again?