Waponyeni watu wamo kifoni, Watoeni walio shimoni; Na aangukaye mumzuie; Ya Bwana Yesu wahubirini. Walio kifoni waokoeni, Mwokozi yuko, wahubirini. Wajapokawia anangojea, Awasubiri waje tobani; Msiwadharau, muwaonyeni; Huwasamehe; wakiamini. Myoyoni mwa ndani, yule shetani Ameyaseta mawazo yao; Lakini kwa Bwana huwa mazima, Tukiwavuta kwa pole hao. Kawaokoeni, wale njiani, Mutimize mapenzi ya Bwana; Na kwa nguvu zake warudi kwake, Kwa subira waonyeni sana.Худосиз яшаб мен О сколько душ блуждают от Бога далеко There's a Great Day Coming Praise, My Soul, the King of Heaven tstạhl ạ̉gẖny lk Ики Киши Тарлада O Seigneur éternel Голјат ҹəнҝə чыхды Gör O'nun Yüce Sevgisini Yo vengo a ti, Señor
Song not available - connect to internet to try again?