Yesu unipendaye Kwako nakimbilia, Ni wewe utoshaye, Mwovu akinijia; Yafiche ubavuni, Mwako maisha yangu; Nifiikishe mbinguni Wokoe moyo wangu. Ngome nyingine sina; Nategemea kwako. Usinitupe Bwana , Nipe neema yako, Ninakuamania Mwenye kuniwezesha; Shari wanikingia, Vitani wanitosha. Nakutaka Mpaji Vyote napata kwako; Niwapo muhitaji, Utanijaz vyako; Nao waangukao Wanyonge wape nguvu; Poza wauguao, Uongoze vipofu. Bwana umeniosha Moyo kwa damu yako; Neema ya kutosha Yapatikana kwako; Kwako Bwana naona Kisima cha uzima; Mwangu moyoni Bwana, Bubujika daima.mkẖlṣy dẖbḥt - hrmạs smyr Я один из них Հայաստան Ունես կարիքը Քրիստոսի unknown Да я спасен спасен я от блужданий Знаю я Solo Gesù مەن السىراپ، جان دۉينۅم قىينالعاندا Бог любви Бог сирот и вдов, с высоты на нас посмотри Merhametli Bir Tanrı
Song not available - connect to internet to try again?