Akifa Yesu nikafa naye Uzima upya huishi naye; Humtazama mpaka nje: Nyakati zote ni wake yeye. Nyakati zote nimo pendoni, Nyakati zote ni uzimani, Humtazama hata atokee, Nyakati zote mimi ni wake. Vita sipigi visivyo haki, Na Bwana wangu hapiganiki; Beramu yake haitwaliki, Napo po pote hila sitaki. Sina mashaka, akawa mbali; Mizigo yote aihimili; Ananituliza Imanweli, Nyakati zote mimi husali. Sina huzuni na mimi sidhii; Simwagi chozi, wala siguni; Sikuti afa, ila kitini Daima hunifikiri mimi. Kila unyonge huusikia; Kila ugonjwa kwake hupoa; Yesu ni mwenye kuniokoa Nyakati zote hunijalia.Эзэний гэр юутай сайхан бэ جەر جۇزىندە زاڭعار كوكتە La Tine la Tine Isuse eu voi veni Қудайсыз өмир Мы открываем небо... شايفينك يارب All'infuori di te The Only One Jesús no vino a condenar تراك 5
Song not available - connect to internet to try again?