Baba yetu aliye Mbinguni Amenifurahisha yakini Kuniambia mwake chuoni Ya kuwa nami Yesu pendoni. Anipenda Mwokozi Yesu, Anipenda, anipenda; Anipenda Mwokozi Yesu, Anipenda mimi. Nimuachapo kutanga mbali, Yeye yu vivyo, hupenda kweli, Hunirejeza kwake moyoni; Kweli yu nami Yesu pendoni. Anipenda! Nami nampenda; Kwa wokovu alionitenda; Akanifia Msalabani Kwa kuwa nami Yesu pendoni. Haya kujua yanipa raha; Kumuamini kuna furaha; Humfukuza mara shetani, Kwona yu nami Yesu Pendoni. Sifa ni nyingi asifiwazo, Moja ni sana katika hizo, Wala siachi, hata Mbinguni, Kwimba, 'Yu nami Yesu pendoni'.dāng nǐ tà shàng zhè tiáo lù Тишина царит в полночи Minnәtdaram Sәnә İsa Бөгүн бис амырап тур бис هيا بنا نهتف Блаженны те кто в доме Твоём رغم القيود ربي موجود Чудный и верный Спаситель Сомненьям меня не взять Белое платье невесты Чистый виссон
Song not available - connect to internet to try again?