Baba yetu aliye Mbinguni Amenifurahisha yakini Kuniambia mwake chuoni Ya kuwa nami Yesu pendoni. Anipenda Mwokozi Yesu, Anipenda, anipenda; Anipenda Mwokozi Yesu, Anipenda mimi. Nimuachapo kutanga mbali, Yeye yu vivyo, hupenda kweli, Hunirejeza kwake moyoni; Kweli yu nami Yesu pendoni. Anipenda! Nami nampenda; Kwa wokovu alionitenda; Akanifia Msalabani Kwa kuwa nami Yesu pendoni. Haya kujua yanipa raha; Kumuamini kuna furaha; Humfukuza mara shetani, Kwona yu nami Yesu Pendoni. Sifa ni nyingi asifiwazo, Moja ni sana katika hizo, Wala siachi, hata Mbinguni, Kwimba, 'Yu nami Yesu pendoni'.Во тьме глубокой где мир мне незнаком Ceasul vremii Od ojczystej naszej ziemi ạsmʿ ṣrạkẖy yạsydy تعليق 4 - أطفال بيحبوا مصر Исо, мен Сени севаман Spre ţara luminii eterne Сохрани 黎巴嫩的香柏树 Пригорнулась до Тебе душа
Song not available - connect to internet to try again?