Baba yetu aliye Mbinguni Amenifurahisha yakini Kuniambia mwake chuoni Ya kuwa nami Yesu pendoni. Anipenda Mwokozi Yesu, Anipenda, anipenda; Anipenda Mwokozi Yesu, Anipenda mimi. Nimuachapo kutanga mbali, Yeye yu vivyo, hupenda kweli, Hunirejeza kwake moyoni; Kweli yu nami Yesu pendoni. Anipenda! Nami nampenda; Kwa wokovu alionitenda; Akanifia Msalabani Kwa kuwa nami Yesu pendoni. Haya kujua yanipa raha; Kumuamini kuna furaha; Humfukuza mara shetani, Kwona yu nami Yesu Pendoni. Sifa ni nyingi asifiwazo, Moja ni sana katika hizo, Wala siachi, hata Mbinguni, Kwimba, 'Yu nami Yesu pendoni'.تعليق 2 Jésus, Jésus, qui peut sonder Let All Mortal Flesh Keep Silence Ce frumoasă-i ţara mea Благословен Господь 每当我想起主钉十架 Csak Istenben nyugoszik Приводишь тьму Ты в трепет O'na Aşığım ná bó de pú táo yuán
Song not available - connect to internet to try again?