Chini ya msalaba Nataka simama; Ndio mwamba safarini, Wa kivuli chema; Ni kweli kwa roho yangu Ni tuo kamili, Tatua mzigo wangu Wakati wa hari. Hapa ni pema sana, Ni ngome kamili; Hapa yameonekana, Mapenzi ya kweli; Kama alivyoonyeshwa Yakobo zamani, Msalaba umekuwa Ngazi ya Mbinguni. Na Yesu msalabani Walimkemea, Alikufa niokoke Niliyepotea; Naona ajabu sana Ya mambo mawili Jinsi alivyonipenda, Nisiyestahili. Atakayeonana, Na Yesu Mbinguni, Njia yake aanzapo Ni msalabani; Wokovu upo hapa tu, Mwingine hapana, Kisha kuna furaha kuu Pamoja na Bwana.طالب حضورك زيك مفيش Апирин Саңа Рәб Әйса nǐ yù jiàn zhǔ le ma بْلا گَلان شا بْبْن Միայն Դու ես Արժանի Pan Jezus chce Rabbimiz Gökleri Ve Yeri Yarattı Даналық Сенинлейкен
Song not available - connect to internet to try again?