Jina lake Yesu tamu; Tukilisikia Hutupoza, tena hamu Hutuondolea. Roho iliyoumia Kwalo hutibika, Chakula, njaani pia; Raha, tukichoka. Jina hili ni msingi, Ngao, ngome, mwamba, Kwa hili napata wingi, Kwangu ni akiba. Yesu, Mchunga, Rafiki Mwalimu, Kuhani, Mwanzo, Mwisho, Njia, Haki, Uzima kifoni. Moyo wangu hauwezi, Kukusifu sana, Ila sifa zangu hizi, Bwana zikubali. Na utakaponiita, Kuja kwako Bwana, Huko kwako sitaacha Kukusifu sana.Sevgi Сильней чем жизнь Господи благослови Бог есть Любовь Salama Ta Allah Kamar Kogi Ce Grande sei o mio Signor Kaulah, ya Tuhan, Surya Hidupku Сенин чексиз сүйүүң жүрөктү жылытат Alleluia Oh Jesús, dulce refugio
Song not available - connect to internet to try again?