Jina lake Yesu tamu; Tukilisikia Hutupoza, tena hamu Hutuondolea. Roho iliyoumia Kwalo hutibika, Chakula, njaani pia; Raha, tukichoka. Jina hili ni msingi, Ngao, ngome, mwamba, Kwa hili napata wingi, Kwangu ni akiba. Yesu, Mchunga, Rafiki Mwalimu, Kuhani, Mwanzo, Mwisho, Njia, Haki, Uzima kifoni. Moyo wangu hauwezi, Kukusifu sana, Ila sifa zangu hizi, Bwana zikubali. Na utakaponiita, Kuja kwako Bwana, Huko kwako sitaacha Kukusifu sana.Bevar meg Jesus Vďaka za Tvoj kríž Коли моє серце Все к лучшему Licht dieser Welt Benim Nefesimsin Ježiš, to meno znie qṣẗ ạlḥb ạlʿjyb Firmanmu, Tuhan, Adalah Kebun Isus e mangaierea mea
Song not available - connect to internet to try again?