Juu yake langu shaka, Yesu namuwekea, Nami sitafedheheka Nikimtegemea. Natumai, natumai, Nnatumai kwake tu; Natumai, natumai, Natumai kwake tu. Juu yake, dhambi zangu; Aniosha kwa damu; Nionekane kwa Mungu, Nisiye na laumu. Juu yake yangu hofu; Kwake nimetulia; Sipotei kwa upofu Njia aning'azia. Juu yake raha yangu; Humuangalia tu; Mwenye kila ulimwengu, Aniruzuku na huu. Juu yake, moyo wangu; Hali yangu na mali; Mimi wake, Yeye wangu, Twapasana kamili.A jó Isten virága Сен Йюдже Месихсин It's Christmas Con Te jyl yṣnʿ ạltgẖyyr Boże Zbawicielu Underfullt Jesus elsket Tutto di me Ким каранлъъ йенди сьойле Ton Roi vient, pauvre
Song not available - connect to internet to try again?