Liko lango moja wazi, Ni lango la mbinguni; Na wote waingiao Watapata nafasi. Lango ndiye Yesu Bwana Wote waingie kwake, Lango! Lango La Mbinguni li wazi. Yesu ndiye lango hili, Hata sasa li wazi, Kwa wakubwa na wadogo, Tajiri na maskini. Hili ni lango la raha, Ni lango la rehema; Kila mtu apitaye Hana majonzi tena. Tukipita lango hili Tutatua mizigo, Tuliochukua kwanza, Tutavikwa uzima. Hima ndugu tuingie Lango halijafungwa, Likifungwa mara moja Halitafunguliwa.Ecazkar Sirr THE DAY THOU GAVEST, LORD Appartengo a te راقمەت، ساعان قۇداي يەم! Kom og gå med meg, til min Faders hus mzmwr 117 - mrnm Rab Benim Çobanımdır 大山记得你 Бракма бени ялнъз сен fy̱ ạlkẖṭyẗ
Song not available - connect to internet to try again?