Bwana Yesu atakuja, Vumilia! Omba, ukiwa na haja, Vumilia! Mbingunu Mungu aliko, Mwamini Mwokozi wako, Nawe utafika huko, Vumilia! Ikikucheka dunia, Vumilia! Mwovu atakuvizia, Vumilia! Hataweza kukushinda, Bwana Yesu akulinda, Roho yako, akupenda, Vumilia! Na ukiwa hatarini, Vumilia! Dhiki nyingi duniani, Vumilia! Vyatupasa kuyakuta, Majaribu na matata, Na Bwana hakutuficha; Vumilia! Adui wakikutana, Vumilia! Na ndugu wakikukana, Vumilia! Zote, zote zitakwisha, Nguvu zote za kutisha Mungu chini atashusha; Vumilia! Moyoni una majonzi, Vumilia! Ndiyo bonde-ya-machozi, Vumilia! Hima tutaandamana, Kwetu Mbinguni na Bwana Tena hatutaachana; Vumilia!نشيدي يعلو بالهتاف На рассвете последнего утра Înălţăm rugile astăzi spre ceruri آتي إليك يا فادي حياتي Å, hvor jeg elsker Jesus Kurtuluş Ezgisi Braman ya con tonco son În veci slăvit fie Domnul Зүрх сэтгэлийг минь нээгээч 在主里有真平安
Song not available - connect to internet to try again?