Mwokozi umeokoa, Nimekuwa wako wewe. Damu imenisafisha. Sifa kwa mwana Kondoo. Utukufu, Aleluya! Sifa kwa Mwana Kondoo! Damu imenisafisha, Utukufu kwa Yesu! Nilijitahidi sana Ila sikupata raha; Bali kwa kumtegemea Nilipata Baraka. Daima namwegemea Damu ikifanya kazi, Nikioga kwa chemichemi Itokayo Mwokozi. Sasa nimewekwa wakfu; Nitaishi kwako wewe: Fahari nashuhudia Ya wokovu wa bure. Nasimama kwake Yesu, Ameponya roho yangu; Ameniondoa dhambi, Anifanye mzima. Nilikuwa kifungoni, Niliteswa na dhambi, Nilifungwa minyororo Yesu akanifungua. Sifa, ameninunua! Sifa, nguvu za wokovu! Sifa, Bwana huhifadhi! Sifa zake milele.İsa geldi bana ʿly̱ ḥsạb ạldm ạnạ dạkẖl Tobě patří čest i sláva نرفض أي عيان هو الرب mjdaⁿạ fy ạlạ̉ʿạly Let the Living Water Flow Sì Gesù mi ama İsa Mesih Dünyamıza Geldi Solo
Song not available - connect to internet to try again?