Ndiyo damu ya baraka ituoshayo wakosa, Kwake Bwana twaokoka, nasi twamsifu sasa; Nimestahili hukumu, siwezi kujitakasa; Nioshe katika damu, takuwa safi kabisa. Safi kabisa; safi kabisa! Nioshe katika damu; Takuwa safi kabisa. Yesu alivikwa miiba, na kuangikwa Mtini, Na maumivu si haba yaliyompata chini. Nataka kijito hicho niende kuoga sasa; Ndicho kinitakasacho, nami ni safi kabisa. Safi kabisa; safi kabisa! Ndicho kinitakasacho, Nami ni safi kabisa. Baba, kweli nimekosa, moyo wangu ni dhaifu; Dhambi ni nyingi kabisa, nipate wapi wokovu? Yesu kijitoni pako, naja naamini sasa; Nioshe kwa damu yako, takuwa safi kabisa. Safi kabisa; safi kabisa! Nioshe kwa damu yako, Nami ni safi kabisa.Их Эзэн жаал хүү چىندىق بئر عانا قۇدايدا اسمان تىرەپ توولورۇ قىرعىزىمدىن Ажойиб иноят Grande e glorioso Signore Мой Бог Ты скала СЪРЦЕТО МИ ПЕЕ ДУШАТА МИ ПЕЕ Io Ti dono il mio cuore Всё дышащее да хвалит Господа КОЙ Е ПОДОБЕН
Song not available - connect to internet to try again?