Ndiyo damu ya baraka ituoshayo wakosa, Kwake Bwana twaokoka, nasi twamsifu sasa; Nimestahili hukumu, siwezi kujitakasa; Nioshe katika damu, takuwa safi kabisa. Safi kabisa; safi kabisa! Nioshe katika damu; Takuwa safi kabisa. Yesu alivikwa miiba, na kuangikwa Mtini, Na maumivu si haba yaliyompata chini. Nataka kijito hicho niende kuoga sasa; Ndicho kinitakasacho, nami ni safi kabisa. Safi kabisa; safi kabisa! Ndicho kinitakasacho, Nami ni safi kabisa. Baba, kweli nimekosa, moyo wangu ni dhaifu; Dhambi ni nyingi kabisa, nipate wapi wokovu? Yesu kijitoni pako, naja naamini sasa; Nioshe kwa damu yako, takuwa safi kabisa. Safi kabisa; safi kabisa! Nioshe kwa damu yako, Nami ni safi kabisa.Pe-oceanul infinit cu valuri تعال يا سيد الفقراء Ժամերը Հաշված Zi de zi clipită de clipită SUNPARNAK NA TA A SI Дай Боже им счастье на многие дни Как олень что ищет воду Sensan Sevgi Rabbim Нужна мне сила Твоя Come, Holy Spirit (Vertical Church Band)
Song not available - connect to internet to try again?