Ndiyo damu ya baraka ituoshayo wakosa, Kwake Bwana twaokoka, nasi twamsifu sasa; Nimestahili hukumu, siwezi kujitakasa; Nioshe katika damu, takuwa safi kabisa. Safi kabisa; safi kabisa! Nioshe katika damu; Takuwa safi kabisa. Yesu alivikwa miiba, na kuangikwa Mtini, Na maumivu si haba yaliyompata chini. Nataka kijito hicho niende kuoga sasa; Ndicho kinitakasacho, nami ni safi kabisa. Safi kabisa; safi kabisa! Ndicho kinitakasacho, Nami ni safi kabisa. Baba, kweli nimekosa, moyo wangu ni dhaifu; Dhambi ni nyingi kabisa, nipate wapi wokovu? Yesu kijitoni pako, naja naamini sasa; Nioshe kwa damu yako, takuwa safi kabisa. Safi kabisa; safi kabisa! Nioshe kwa damu yako, Nami ni safi kabisa.Kiranya Anug'rah Kristus 오라 우리가 여호와의 พระหัตถ์ของพระเจ้าห้าวหาญนัก Невеста IX. Prowadź, prowadź mnie Sam Taký, aký som في الأفراح Кечир мени, Теңир, сурайм кечирим Мы к Тебе идём بتنادي علي
Song not available - connect to internet to try again?