Sauti sikilizeni Za waimbao juu, 'Aleluya, Aleluya, Aleluya, mkuu!' Wako makundi-makundi Kama nyota wang'ara, Kwa makuti ya mitende, Na meupe wamevaa. Wazazi na manabii Wafanyaji wa njia; Mashahidi, waandishi, Nao wafalme pia! Mabikira kina-mama, Wajane wa kusali, Waimba wakikutana 'Msifunu Imanweli'. Watu toka huzunini Wameosha na nguo, Ni kwa damu yake Yesu; Maonjo, mbali nao! Walitekwa, walikatwa Hata kwa misumeno, Kwao kifo na shetani Walishindiwa mno. Mungu mumo mwake Mungu, Nuru mumu mwa nuru, Kwa kufungamana mwako Tutaishi mahuru; Tujalize, Imanweli, Kujaa kwako wewe Mungu Baba, Mungu Mwana, Mungu Roho, tunawe.rby sbyt qlby Ты мой Бог Pintu Gerbang Terbukalah Таныг магтъя Слава Тобі lmạ dʿạny rby Sevgisən Radosťou dnes Cirkev spieva, nebo plesom sa rozlieha kạn ḥkm ạlmwt ʿly Room at the Fountain
Song not available - connect to internet to try again?