Sauti sikilizeni Za waimbao juu, 'Aleluya, Aleluya, Aleluya, mkuu!' Wako makundi-makundi Kama nyota wang'ara, Kwa makuti ya mitende, Na meupe wamevaa. Wazazi na manabii Wafanyaji wa njia; Mashahidi, waandishi, Nao wafalme pia! Mabikira kina-mama, Wajane wa kusali, Waimba wakikutana 'Msifunu Imanweli'. Watu toka huzunini Wameosha na nguo, Ni kwa damu yake Yesu; Maonjo, mbali nao! Walitekwa, walikatwa Hata kwa misumeno, Kwao kifo na shetani Walishindiwa mno. Mungu mumo mwake Mungu, Nuru mumu mwa nuru, Kwa kufungamana mwako Tutaishi mahuru; Tujalize, Imanweli, Kujaa kwako wewe Mungu Baba, Mungu Mwana, Mungu Roho, tunawe.Nech sa veselia Entrons dans sa présence Nie ma innego เยซู กลับฟื้นพระชนม์ Preghiera Teba dnes chválime Da si nu, nu si da Ты - мой ангел Воспой انت الملك يا يسوع
Song not available - connect to internet to try again?