Sauti sikilizeni Za waimbao juu, 'Aleluya, Aleluya, Aleluya, mkuu!' Wako makundi-makundi Kama nyota wang'ara, Kwa makuti ya mitende, Na meupe wamevaa. Wazazi na manabii Wafanyaji wa njia; Mashahidi, waandishi, Nao wafalme pia! Mabikira kina-mama, Wajane wa kusali, Waimba wakikutana 'Msifunu Imanweli'. Watu toka huzunini Wameosha na nguo, Ni kwa damu yake Yesu; Maonjo, mbali nao! Walitekwa, walikatwa Hata kwa misumeno, Kwao kifo na shetani Walishindiwa mno. Mungu mumo mwake Mungu, Nuru mumu mwa nuru, Kwa kufungamana mwako Tutaishi mahuru; Tujalize, Imanweli, Kujaa kwako wewe Mungu Baba, Mungu Mwana, Mungu Roho, tunawe.Te Loamos, ¡Oh Dios! Kde si, môj premilý Pane a Kriste Na Golgote stíš sa, stíš! الاحترام علينا واجب qdmwạ lyhwh yạ ạ̉bnạʾ ạ̹lwhym Я жажду Господи прощенья GLORIFY YOUR NAME Póki mego życia nlt ạlḥyạẗ ạlạ̉bdyẗ Umidvor
Song not available - connect to internet to try again?