Sauti sikilizeni Za waimbao juu, 'Aleluya, Aleluya, Aleluya, mkuu!' Wako makundi-makundi Kama nyota wang'ara, Kwa makuti ya mitende, Na meupe wamevaa. Wazazi na manabii Wafanyaji wa njia; Mashahidi, waandishi, Nao wafalme pia! Mabikira kina-mama, Wajane wa kusali, Waimba wakikutana 'Msifunu Imanweli'. Watu toka huzunini Wameosha na nguo, Ni kwa damu yake Yesu; Maonjo, mbali nao! Walitekwa, walikatwa Hata kwa misumeno, Kwao kifo na shetani Walishindiwa mno. Mungu mumo mwake Mungu, Nuru mumu mwa nuru, Kwa kufungamana mwako Tutaishi mahuru; Tujalize, Imanweli, Kujaa kwako wewe Mungu Baba, Mungu Mwana, Mungu Roho, tunawe.نسبحك ونباركك mạdmt fy sfynty Творец Непостижимый wạḥd ạ̹tnyn tlạtẗ Muy triste vagaba Biricik Oğlun, Günahsızdır hạfḍl ạ̉gẖnylk Иса мен сені сүйем Ozod qiladi Iso Her şey O'nun aracılığıyla var oldu
Song not available - connect to internet to try again?