Yesu nakupenda, U mali yangu, Anasa na dhambi sitaki kwangu; Na Mwokozi aliyeniokoa, Sasa nakupenda, kuzidi pia. Moyo umejaa mapenzi tele Kwa vile ulivyonipenda mbele, Uhai wako ukanitolea Sasa nakupenda, kuzidi pia. Ulipoangikwa Msalabani Tusamehewe tulio dhambini; Taji ya miiba uliyoivaa, Sasa nakupenda, kuzidi pia. Niwapo hai, niwapo maiti, Kupendana nawe kamwe siachi; Hari za kifo zikinienea, Sasa nakupenda, kuzidi pia. Mawanda mazuri, na masikani Niyatazamapo huko Mbinguni, Tasema na taji nitakayovaa Sasa nakupenda, kuzidi pia.Keď zora sfarbí zem Nulla qui in terra sydy yạ qdyr kn rby أنا أنا مبسوط Кровь Христа You, Whose Name is Holy lyh thtm wlyh btkẖạf Jesteś o Panie wśród nas Һаллелуја Ci sarà
Song not available - connect to internet to try again?