Aliteswa, aliteswa, Msalabani Yesu aliteswa, Dhambi zangu ameziondoa, Mahali pangu aliumizwa. Alikufa, alikufa, Msalabani Yesu alikufa, Kwa kifo chake nakombolewa, Kwa kuwa Yesu alinifia. 'Kafufuka, 'kafufuka, Kaburini Yesu alitoka, Nami nimewekwa huru pia, kwa kuwa Yesu alifufuka. Yuko hai, yuko hai, Mbinguni anaishi Mwombezi, Daima huniombea mimi, Kwa kuwa Yesu adumu hai. Atarudi, atarudi, Siku moja Yesu atarudi, Na tutamwonapo tutafurahi, Kwa kupelekwa kwake Mbinguni. Sifa kwake, sifa kwake, Mbinguni na huimbwa milele, Kwa furaha, masifu, na shangwe, Tutamwimbia Yesu milele.Náš chválospev nech zaznie Levati o Dio Kun Ji Shela A Ke Yi, Halleluya! İçimde Taştan Yürek Var بنلاقيك وسط المصاعب Sosită e iar primăvara Гэрэлт дэнлүү Огнена Вяра Din mulţimea de cuvinte Он держит весь мир в Своей руке
Song not available - connect to internet to try again?