Aliteswa, aliteswa, Msalabani Yesu aliteswa, Dhambi zangu ameziondoa, Mahali pangu aliumizwa. Alikufa, alikufa, Msalabani Yesu alikufa, Kwa kifo chake nakombolewa, Kwa kuwa Yesu alinifia. 'Kafufuka, 'kafufuka, Kaburini Yesu alitoka, Nami nimewekwa huru pia, kwa kuwa Yesu alifufuka. Yuko hai, yuko hai, Mbinguni anaishi Mwombezi, Daima huniombea mimi, Kwa kuwa Yesu adumu hai. Atarudi, atarudi, Siku moja Yesu atarudi, Na tutamwonapo tutafurahi, Kwa kupelekwa kwake Mbinguni. Sifa kwake, sifa kwake, Mbinguni na huimbwa milele, Kwa furaha, masifu, na shangwe, Tutamwimbia Yesu milele.النضافة لخير الإنسان ھۆكۈمرانىم سەن Среди невзгод сомненья и ненастья أنا هنا لأعبدك رنمي للرب يا كل الأرض yạ kẖạṭy̱ ạʿrf ṭryqk تأمل 3 Ուրախ սիրտը օգտակար พื้นฟ้าสวรรค์ประกาศพระบารมี محتاج أن أتعلم
Song not available - connect to internet to try again?