Aliteswa, aliteswa, Msalabani Yesu aliteswa, Dhambi zangu ameziondoa, Mahali pangu aliumizwa. Alikufa, alikufa, Msalabani Yesu alikufa, Kwa kifo chake nakombolewa, Kwa kuwa Yesu alinifia. 'Kafufuka, 'kafufuka, Kaburini Yesu alitoka, Nami nimewekwa huru pia, kwa kuwa Yesu alifufuka. Yuko hai, yuko hai, Mbinguni anaishi Mwombezi, Daima huniombea mimi, Kwa kuwa Yesu adumu hai. Atarudi, atarudi, Siku moja Yesu atarudi, Na tutamwonapo tutafurahi, Kwa kupelekwa kwake Mbinguni. Sifa kwake, sifa kwake, Mbinguni na huimbwa milele, Kwa furaha, masifu, na shangwe, Tutamwimbia Yesu milele.Kipak Lothei Kei Puoi أوهام على الصليب 充满信心充满盼望 Tu Mirada ۅمۉر قىسقا جايقى تۉندۅي ṣnʿ ạlrb wlymẗ Why Don't You Let Go Christ nous précédant మాట్లాడే దేవా నా యేసయ్యా
Song not available - connect to internet to try again?