Aliteswa, aliteswa, Msalabani Yesu aliteswa, Dhambi zangu ameziondoa, Mahali pangu aliumizwa. Alikufa, alikufa, Msalabani Yesu alikufa, Kwa kifo chake nakombolewa, Kwa kuwa Yesu alinifia. 'Kafufuka, 'kafufuka, Kaburini Yesu alitoka, Nami nimewekwa huru pia, kwa kuwa Yesu alifufuka. Yuko hai, yuko hai, Mbinguni anaishi Mwombezi, Daima huniombea mimi, Kwa kuwa Yesu adumu hai. Atarudi, atarudi, Siku moja Yesu atarudi, Na tutamwonapo tutafurahi, Kwa kupelekwa kwake Mbinguni. Sifa kwake, sifa kwake, Mbinguni na huimbwa milele, Kwa furaha, masifu, na shangwe, Tutamwimbia Yesu milele.Soylar yigʻilsa koʻl boʻladi rạḥty fyk Přijď již, přijď Duchu Stvořiteli Кръвта на Господа Sen Bilan Bir Kun Столько песенных строк прославляют Творца Bənzəmək istərəm mən Sənə, Rəbbim Chcem len tvojím, Pane لا تخف لأني فديتك قدس الأقداس هو ليك
Song not available - connect to internet to try again?