Aliteswa, aliteswa, Msalabani Yesu aliteswa, Dhambi zangu ameziondoa, Mahali pangu aliumizwa. Alikufa, alikufa, Msalabani Yesu alikufa, Kwa kifo chake nakombolewa, Kwa kuwa Yesu alinifia. 'Kafufuka, 'kafufuka, Kaburini Yesu alitoka, Nami nimewekwa huru pia, kwa kuwa Yesu alifufuka. Yuko hai, yuko hai, Mbinguni anaishi Mwombezi, Daima huniombea mimi, Kwa kuwa Yesu adumu hai. Atarudi, atarudi, Siku moja Yesu atarudi, Na tutamwonapo tutafurahi, Kwa kupelekwa kwake Mbinguni. Sifa kwake, sifa kwake, Mbinguni na huimbwa milele, Kwa furaha, masifu, na shangwe, Tutamwimbia Yesu milele.In alto volerò Lacrimile de durere yạ ạbny bḥbk أما أنا أنا وبيتي - بصوت الراحل نجيب إبراهيم Jezus objawione serce Boga Jezus jak cudowny to Pan Can bəxş eylədi Դու Միայն Դու كم أتمنى Megragadtál, Jézus Krisztus
Song not available - connect to internet to try again?