Kale nilitembea Nikilemewa dhambi Nilikosa msaada, kuniponya mateso. Usifiwe Msalaba! Lisifiwe kaburi! Linalozidi yote, Asifiwe Mwokozi! Hata nilipofika, Mahali pa Msalaba, Palinifaa sana, Sitasahau kamwe. Hicho ndicho chanzo, Cha kufurahi kwangu. Hapo ndipo mzigo, Uliponituliwa. Panapo msalaba, Kinatolewa cheti, Cha kuingia Mbinguni, Kisicho cha kanisa. Yule Bwana mjinga, Likwenda bila cheti, Kitumai kwingia, Kama walio nacho. Lipofika langoni, Akaulizwa cheti, Cha kumwonyesha Bwana, Akakutwa hanacho. Lituhuzunishalo, Ni ninyi msio nacho, Kuwa kama mjinga, Kwa siku ya arusi! Ubavuni mwa Yesu, Mlitokea damu, Chemchemi ya uzima, Itakasayo roho. Jitahidi wingie, Damuni mwa Mwokozi, Utafutiwa dhambi, Toka rohoni mwakoJak Sam, Panie, chcesz, niech będzie Gewagte Liebe Hier bist du richtig mtsẖạl jwh ạlʿyn Худованднинг Руҳи Менга ёр (анъанавий) Tonga ny hariva Счастлив свободен лишь тот Моё имя записано на ладонях You're my provider Хак олан не варса
Song not available - connect to internet to try again?